Kuamini Yesu Kristo
Si kila imani


Bila shaka, unapatikana miongoni mwa wale wanaoamini Mungu. Ni yule Mungu unayemuona kwa namna yako: “Mungu Mwema”, anayesamehe makosa yako, anayekuwa mbali kwa makosa ya wengine.Mungu yule anayehakikisha uwepo wake kwa fahamu lako, ila unayependa kuwa mbali yake iwezekanapo.
Biblia inasema:
“Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na watetemeka.” (Yakobo 2.19).
Hiyo ndiyo hatari inayowapata wale wote wanaotosheka na kuamini Mungu . Wengine wanaongeza kusema: nina imani yangu, na dini yangu, na ninafanya hata kazi zote za zehebu yangu…Fanya angalisho! Imani ni neno pana, linaloweza kumaanisha maneno mengi kwa mara moja, na hivi ni lenye hatari. Kila mtu ana imani yake, yenye haijulikane vizuri : anamoweka karibu atakacho chochote.
Si dini
Dini ni neno rahisi, lisilokuwa na matatizo, linakusanya mazowezi yote ambayo mtu anaweza kuheshimu bila kujitakia mwenyewe. Ubatizo, kuvunja mkate, ndoa, mazishi : vitu vine vinavyotosha ili uwe na dini ya kuheshimiwa. Kweli, hamuna magumu, yatosha kutoa siku ine za maisha – na tunaona ya kwamba ile ya ine si yetu – na kufanya sherehe siku tatu za kwanza katika jamaa, kula vizuri na kupana zawadi. Na mwisho unakuwa wala unabaki kuwa mukristo muzuri. Ni rahisi kweli, sivyo ? Ni udanganyifu mtupu !
Imani ya kweli
Ulizo linalofaa kuuliza ni hili : «Ni nani tunayeamini?» Linatupeleka mbali kuliko tunavyowaza. Tukiamini Mungu wakati anaposema, ndipo Biblia, Biblia yote inakamata mamlaka juu yetu kwa sababu inajishuhudia kwa uhakika kuwa : Neno la Mungu.
Mungu anasema. Anayoyasema si kweli ? Si yeye mwenyewe anayeweza kusema ukweli ? Ukiwa na shaka kwa neno lake, Biblia, ni kumfanya kuwa mwongo.
«Asiyemwamini Mungu amemufanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemushuhudia Mwanae» (1 Yoane 5.10).
Mungu anashuhudia Mwanae katika Neno lake na mtu ana uajibu wa kupokea ushuhuda huo, kupokea Mwana wake. Hiyo ni tofauti na imanitupu, na sura ya dini tupu; hii ndiyo inaitwa Imani.
« Imani huja kwa kusikia, na kwa kusikia Neno la Mungu.» ( Waroma 10.17) .
Msimamo wa imani
Hakuna imani ya umati wala ya jamaa. Imani ni msimamo wa kibinafsi unaoongoza kila mtu kuchukua kwa unyenyekevu nafasi anayotayarishiwa na Neno la Mungu : nafasi ya kiumbe mbele ya Muumbaji na nafasi ya mwenye zambi mbele ya Mungu Mtakatifu.
Kwa kuwa ni Mungu ndiye anasema, imani inanyamanzisha akili na mawazo yote ya mwanadamu pia hisia zake. Imani inapokea ile yote ambayo Mungu anasema juu ya mtu na kwa mtu. Inapokea ile ambayo Mungu anasema juu ya Yesu Kristo ; inakubali kufundishwa jinsi gani hali ya moyo wa mtu ilivyo – mbaya na usiyoweza kuponywa – na jinsi gani hali ya moyo wa Mungu ilivyo, inajaa upendo, huruma, musamaha.
Imani ina akili, inavumilia, inatii. Inahukumu yaliyopita, inapokea ya leo na kuelekeza macho yake juu ya mambo yanayokuja ambayo yatakamilisha haki yake.
Uhakika wa imani
Imani inatambua haki za Mungu juu ya dunia na juu ya kila mtu aishie ndani yake. Inafundishwa na Mungu – siyo kwa maagizo ya wanadamu – ya kwamba yeye ni Mungu wakuhukumu lakini vilevile yeye ni Mungu anayetoa neema.
Imani ni kumjua binafsi Mungu aliyejifunuwa katika Mwana wake, kumjua Mungu anayesema, anayesikia na kujibu. Imani ni uhusiano ulio hai na huyu Mungu , aliyegeuka Baba yetu, na pamoja na Bwana Yesu Kristo mwenye upendo na amri. Imani inatosha uhakika huu ndani ya Neno la Mungu.
« …lile neno la imani tunalolihubiri ni : Kama ukikiri kwa kinywa chako yakuwa Yesu ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua toka wafu, utaokolewa!»
«Basi tukiisha kuhesabiwa haki kwa njia ya imani, tuna salama kwa Mungu , kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo» (Waroma 10.8-9 na 5.1).
«Lakini pasipo imani, haiwezekani kumpendeza - Mungu» (Waebrania 11.6).
Imani hiyo, unayo?
Unaweza kutuandikia kwa anwani hii:
Centre de Diffusion de la Bible
B.P. 40 GOMA
24 BUTEMBO
Upashaji huu hauna shabaha nyingine isipokuwa ile ya kukuletea ujumbe ambao Mungu anatumia kila mtu: Biblia.
Hauna uhusiano na zehebu mbalimbali ambazo zina shabaha ya kukokota watu ndani ya vikundi vyao.
Tafazali usitupe barabarani!
Asante.