UTIMIZA UTENDAJI WA USHIRIKA KATIKA MAKANISA YA PAHALI
KANISA LA PAHALI


Magawanyiko mengi ya ukristiano inatuhuzunisha. Hasa ambayo inahuzunisha sana ni ile magawanyiko katikati ya waamini wanaojidai kukusanyika kwa jina la Bwana. Maandiko matakatifu inatuonya kwa ‘kuchunga umoja wa Roho kwa kamba ya amani ‘ (Waefeso 4:3).
Maana yake umoja unafanyika pamoja na wote washirika wa mwili wa Kristo. Alakini tunapashwa kuchunga (kwa sababu iko tayari sasa) umoja wa Roho ndani ya utii wa Neno la Mungu, kama hatutaki kupatwa na hatari mbili hizi:
Mawazo pana sana yenye haitengenee muzuri ao mawazo membamba vilevile yenye haitengenee muzuri. Tunataka ndani ya sura hii ya sasa kuheshimu swali hii : Pamoja na nani
Tunaweza kuwa na ushirika na umoja wa mwili wa Kristo kwa meza ya Bwana?
Kitu ya kwanza kutengeneza ni kujua nani ni kiungo cha kanisa. Kufatana na Neno la Mungu ni wale waliomugeukia Mungu, wakikiri zambi zao na wanaamini Bwana Yesu kama ndiye Mwokozi wao, Yeye ambaye alipata hukumu ya Mungu juu ya musalaba kwa ajili ya kufunika zambi zao. Kwa ajili ya, kila mumoja wao anahakikishwa na wokovu wake na anajua ya kwamba yeye ni mwana wa Mungu juu ya musingi wa Maandiko (1 Wakor 6 :19 na Waef 1 :13) wana uhakika kwamba Roho Mutakakatifu anakaa ndani yao. Tutaweza kutumia mara hiyo jina la ‘ waamini ‘ kwa watu wa namna ile.
Kama kwa mwanzo wa kanisa, kuna vile leo waamini ambao katika pahali mbalimbali wanaonyesha kwa njia ya meza ya Bwana umoja wa mwili wa Kristo. Swali la pili linaulizwa sasa : Ni nani anakuwa mumoja wa kanisa la pahali ? Jibu ni ya maana sana : Ni waamini wote wa pahali ile wawe pale ao hapana kwa kuvunja mukate. Kwa kushiriki kwao kwa mukate mumoja, wale ambao wanakuwa pale wanaonyesha umoja wao pamoja na waamini wengine wote, yaani vile pamoja na waamini wenye kukua ndani ya mazehebu vilevile .
KUPOKELEWA KWA MEZA YA BWANA
Ni nani anaweza kushiriki kuvunja mukate kwa meza ya Bwana ndani ya kanisa ya pahali namna ile ? Tuliona kwa sura ya 1 mpaka 3 ya barua hii tabia muhimu ambazo zinaruhusu kupokea waamini wanaojulikana namna ile kwa meza ya Bwana :
- Hawaishi wao wenyewe katika ubaya (1Wakor 5) ao mafundisho mabaya (Wag. 5 :9-10 ; 1 Yoani 4 :1-3 ; 2 Timoteo 2 :17-18)
- Hawa kujichafua, wakijua ao apana, kwa ushirikiano binafsi na wa inje kwa matendo ya dini ambayo inafanya ushirika wa meza ya kuabudu pahali ubaya unavumiliwa. Wao wanaonekana sasa ndani ya ushirika na ubaya, kwa sababu kwa kufanya hivi wanajifananisha pamoja na misingi ambayo inaambatana na hiyo meza ya ushirika (ona ile ambayo tulizungumuzia kwa sura ya 3 yaambatana na 1 Wakor 10. Tukumbushe pia mambo mawili ya Matendo 15 :20 na 29 pale ushirika wa kibinafsi na inje pamoja na ubaya - jinsi ya kukula kwa ile ambayo ilitolewa kwa sanamu - iko hakika uchafu).
- Hawachafuke kwa njia ya kuambatana na wanajua pamoja na watu ambao ubaya ao mafundisho mabaya imeonekana wazi, lakini wanakataa kuyahukumu (1 Wakor 5, 2 Yoani 10 :11)
Kushiriki meza ya Bwana haitaisha tu kwa kanisa la pahali ambalo limekamata mpango ya kupokea mutu. Hii kanisa iko kabisa na mamlaka ya kupokea mutu, lakini pale waamini wanakusanyika kwa jina la Bwana (Matayo 18 :20), waamini wanafanya hivi na nia ya kuonesha umoja wa mwili wa Kristo kwa meza ya Bwana (1Wakor 10 :17). Tunapashwa tena kutia mukazo juu ya umoja wa mwili wa Kristo na juu ya uhusiano katika makanisa ya pahali yanayokuwa na hamu ya kuonesha umoja huo ili kwa namna ile umoja wa Roho uchungwe kimatendo. Hata kama makanisa ya pahali yanajitawala yenyewe na yana mamlaka yake kila moja katika pahali pake,ile haimaanishe kwamba makanisa ziko huru zingine kwa zingine. Mipango, sawa kupokea mutu kwa ushirika wa meza ya Bwana kwa mufano, ikikamatwa kwa kanisa la pahali, inahusu zingine makanisa. Hii agizo ya musingi inatia mkazo juu ya mamlaka makubwa ya kila kanisa la pahali : Mipango ambayo imekamatwa inapashwa kuwa kwa jina la Bwana na kwa namna hii ikiambatana na Neno la Bwana. Ni muhimu, wakati wa kumata mpango, uwe na hakika kwamba umuhimu wake utaendelea mpaka zingine makanisa ya pahali kwa sababu kuenea kwa mpango wa kanisa la pahali unaendelea mpaka dunia yote (Mathayo 18 :18).
Ukubali huu, ambao unaanjishwa juu ya kweli ya umoja wa mwili wa Kristo, utatuchunga kwa kutenda juu juu. Kila kanisa la pahali linapaswa kutenda kwamba linasimamia kwa pahali fulani mwili wa Kristo (1Wakor12 :27) na vile mwili wa Kristo, linatenda juu ya mwili muzima.
Makanisa zingine ya pahali watatambua mipango ambayo imekamatwa kwa sababu :
1. Wanatambua Bwana mumoja
- Kwa jina ambalo wanakusanyika, tena
- Yeye, kwa kuwa kwake ndani ya kanisa inaonyesha nguvu ya mpango ambao ni kwa mapenzi yake (1Wakor 5:4) na analeta mamlaka kwa mipango yake (Mathayo 18:18 na 20).
2. Wanatambua Roho mumoja kwa njia yake Mungu ameweka umoja kwa utukufu na kwa njia yake waamini wanaunganishwa ndani ya mwili mumoja wa Kristo, kichwa kimetukuzwa mbinguni.
Roho hiyo inakataa kwa kila tabia ao kitendo visivyo vya kiroho (Wagal 5:16 na kuendelea) kwa viungo vya mwili wa Kristo ambavyo vinaitwa kwa kuchunga umoja wa roho.
3. Wanatambua mwili mumoja ambao kila kanisa ni sehemu yake, kila moja halifanywe sasa kuwa huru na kujitegemea.
Kama mipango ambayo imekamatwa haitambulikane, hivi ni kukataa, ndani ya matendo, mamlaka ya Bwana (kufwatana na 1. ya juu) pamoja na umoja na ushirika zenye zinaonyeshwa kwa meza ya Bwana. Kama mara nyingi manunguniko yanatokea, ikiambatana na maandiko, kwa ngambo ya ukweli wa mpango, zingine makanisa (yenye inakuwa karibu) zinapashwa sasa kujitaabisha na mpango huu ndani ya unyenyekevu kwa Bwana. Sasa, si mara tu kanisa linatambulikana kama linakusanyika kwa jina la Bwana, makanisa, vile sawa watu, wanafungwa na mipango ambayo linakamata kwa jina la Bwana. Kukataa ile (mipango) inaitwa, ndani ya Agano la kale, kutenda na * majivuno* ao * kiburi* (kumbukumbu la Torati 17:8 mpaka 13).
KUFANYA TENDO LA USHIRIKA
Kusanyiko nyingi ulimwenguni kote zinatambua nyayo za msingi wa ushirika na wa umoja wa kanisa ambazo zinaonyeshwa kwa meza ya Bwana. Wanajisikia kufungwa wengine kwa wengine kwa namna ya upekee, bila hata mawazo yao yawakumbushe kwamba wanafanya wao peke kanisa. Badala yake, wako na uhakika kwamba kila siku ya kwanza ya juma, wanaonesha, kwa kuvunja mukate, umoja wao pamoja na waamini wote wa pahali na wa ulimwengu muzima.Urafiki wa karibu wa kusanyiko hizi unaonyeshwa kwa kutambua kwa lingine na lingine mipango yao (sawa kupokea ao kufunga) na kwa barua zao za ushuhuda za wengine na wengine (2 Wakor 3:1). Makanisa hiyo ya pahali huunganishwa juu ya musingi wa umoja wa mwili wa Kristo, yanaunganishwa juu ya uwanja wa kufanya kitendo cha ushirika. Vifungo hivyo vya ushirika vinawezesha kuonesha umoja wa mwili wa Kristo ndani ya utakatifu na ndani ya usafi.
Ile haina maana kwamba kupokelewa kwa meza ya Bwana kunaisha kwa wale waliopokelewa ndani ya makanisa yale, kama ingekuwa hivi, makanisa yangejifanya kuwa kikundi ambacho kinajifunga, kikiwa na hali ya kujitenga. Inapashwa kukuwa na uwezo wa kupokea waamini wale ambao hawayavunja mukate pale mpaka pale. Kanisa ambalo linapatikana kukabiliana na gumu sawa ile linapashwa kila mara kutafuta mapenzi ya Bwana kwa ngambo ile. Wakati ya kutosha ni ya lazima ili ndugu wawili ao watatu wazungumuze kwa jina la kanisa la pahali pamoja mutu ambaye anahusika, wakikumbuka kanuni tatu za muhimu za kila kupokelewa. Wataweza hivi kujifunja namna ya kumujua na kupata uhakika wa kutosha mbele ya kutangaza maoni yao kwa kanisa amboyo peke yake ina mamlaka ya kuamua kwa jina la Bwana. Hata hivi kanisa la pahali kwa jumla inadumu na mamlaka ya kupokea mutu yule ambaye ndugu zake walizungumuzia.
Fasi zingine, katika dunia muzima kunapatikana vikundi vya kusanyiko ya pahali vyenye vinatenda kukusanyika kwa jina la Bwana, lakini vinasadiki kukuwa huru vingine kwa vingine. Hii ndiyo kukataa umoja wa kanisa, mwili wa Kristo. Udanganyifu namna ule inapeleka kwa hali ya uhuru ao kwa hali ya uvuguvugu wakati inahitajika kutambua mipango ya zingine kusanyiko. Katika vingi vya vikundi hivi, wanatia mbele mamlaka ya kibinafsi peke yake ya wenye kuvunja mkate. Vingine vinatia mpaka upana wa ushirika kwa wale wenye walibatizwa na kupokelewa katikati yao.
KUCHAFUKA KWA NJIA YA MUUNGANO
Wakati mwamini anatoka kwa kusanyiko namna zile, inaomba wakati wa mazungumuzo ionekane wazi kwamba ni kwa moyo safi na kwa nia nzuri anataka kushiriki kwa mkate mumoja pamoja na wale wanaoamini kwamba umoja huo wa kanisa unaishi juu ya ulimwengu na tena kuvunja mkate ndio ushuhuda wake.
Ni ya maana sana kukuwa na mazungumuzo ambayo inaongeza mapendo na mukazo, ndani ya kulinganisha mara ngapi uchafu unaweza kujiingiza mbio kama mwamini huyu:
- anataka kuweza kushiriki meza ya Bwana chini ya mamlaka yake yeye mwenyewe;
- ana ukubali kwamba uchafu unakuwa mara moja wakati unakubali ubaya binafsi na apana wakati mutu anataka hali ya uvuguvugu kwa kulingana na ubaya. Hii ukubali inapatikana ndani ya mengi zaidi ya kusanyiko huru.
- anasimamisha ukubali wake juu ya misingi ya uhuru wa kila kanisa la pahali. Ttukamate mufano wa kusanyiko (A) pale ambako ubaya ao mafundisho mabaya inajulikana na kuvumiliwa. Kwa namna hii, kusanyiko hii imechafuka (kufatana na 1 Wakor. 5) na hizi hali zinaweza kuonekana.
a. kusanyiko la pili (B) linapokea mutu wa kusanyiko lenye linachafuka (A) na wanajua muzuri uvumilivu ambao unakaa kufatana na ubaya. Hii hali ya uvuguvugu kwa ngambo ya uvumilivu wa ubaya unachafua vilevile kusanyiko (B) lenye kupokea.
b. kusanyiko la tatu (C) linakataa kupokea mutu wa kusanyiko linalochafuka (A).
c. isitoche inaweza fika nyuma ya hapo waamini wa kusanyiko (C) ambao hawavumilie ubaya, wanashiriki kuvunja mkate pamoja na waamini wa kusanyiko (A ao B) ndani ya kusanyiko lingine (D).
Namna hizi zinakataa kimatendo umoja wa mwili wa Kristo na zinaleta machafuko ndani ya nyumba ya Mungu. Kila moja ya wale wanaopatikana ya hali ile ya uchafu kwa ubaya, wakiwa wanajua yote wanakamata hali ya uvuguvugu, inawachafua vilevile. Gumu ambayo inazungumuziwa hapa ni ile ya ushirika makusudi na ubaya wa namna ya zamiri ao mafundisho mabaya ambayo inafanya mutu “mbaya“ kufwatana na 1 Wakor 5.
Kwa hivi, wakati makanisa ya pahali zinataka kufanya ushirika wenyewe kwa wenyewe juu ya musingi wa uhuru, kunaweza kuwa kujuta juu ya ukali wa mapigo mutu na vile juu ya matokeo ya usafi ya makanisa.
Si hivyo tu kwa ulimwengu wa sasa, lakini vile siku hizi za leo, ndani inchi nyingi, kusanyiko namna zile zinaonekana, pale waalimu wa uwongo wanavumiliwa, na sasa wanafundisha mafundisho mabaya juu ya uutu wa Kristo, uongozi na mamlaka ya biblia, ao wanajiunga na mafundisho ya wokovu wa ulimwengu.
Kupokelewa kwa muda haipashwi kuacha kuwaza kama tunakubali na misingi yenye imebaki ndani ya kusanyiko ao kikundi ambacho mutu husika ni mumoja wake. Hii ni ya muhimu juu ya kukinga uzaifu wa misingi ya biblia yenye tunatumika katikati yetu. Itakuwa jambo sawa vile kama tunashiriki kuvunja mkate ndani ya zingine kusanyiko. Hatukujifunja kwa 1 Wakor 10 kwamba ushirika huo unamaanisha kuingizwa ndani ya misingi inayofwatwa ndani ya kusanyiko. Swali gumu ambalo linaulizwa ni kujua kama tunapashwa kujifananisha na musingi wa upana ao huru, ijapokuwa ile inapeleka mbio kwa hali ya uvuguvugu kwa namna ya ubaya. Ndugu Darby aliandika kuhusu makanisa pana ao huru :
Ninapenda kutaja ndugu W.Kelly juu ya yule ambaye anaweza kujiuliza kama hatupatie kwa uraisi sana maneno ya “pana” ao “huru” kwa kundi zingine:
Ingekuwa heri kusema hakika ni pahali gani wakristo wale wa kawaida wanakuwa wote ambao kutokukamilishwa moja tu, ingekuwa, inafanana, kwamba wengine wanawaita wandugu wapana. Kama ingekuwa kwa ufupi jina na apana uhakika, wangeweza kuuliza na kupokea msaada ili kwa kuchungwa, na mafundisho makamilifu zaidi ya kweli, kwa mtego ambao juu yake wanawekwa. Ni nani hatawekwa kwa kujibu mwito kwa msaada ndani ya njia ile? Tumetoka sasa hivi kujulisha pamoja na kundi namna ile, na Mungu alipendezwa kusawanisha njia yao. Wako ndani ya ushirika wa furaha, wanakusanyika kwa jina la Kristo, badala ya kutupwa huko na huko bila shina ao musingi ya Mungu. Lingine ambalo lilidai sasa kukuwa hivi, lilionesha kukuwa kwa mwisho “wandugu wapana” (Bible Treasury, vol. 16, ukurasa 208).
Katika hali hizi zote, kunapashwa kukuwa kukutana ndani ya mapendo na unyenyekevu, ikikamata musingi wa utii kwa neno la Mungu na ndani ya kujiweka kwa kuchunga umoja wa Roho kwa kifungo cha salama. Ni muhimu kuchunguza kama mwamini namna ule anaweza kutaja jina la Bwana na moyo safi. kama anaonekana kwa kuhukumu kwa moyo wake wote kile ambacho ni tofauti na Neno la Mungu, kazi yetu ni kusaidia kwa kuuweka usikie misingi isiyo ambatana na maandiko na kwa mambo ambayo inaweza kubaki ndani ya zehebu lake ao kundi lake, bila kutaka kumushurutisha mambo fulani kama kanuni.
“Neema ya Bwana Yesu Kristo na upendo wa Mungu na umoja wa Roho Mtakatifu, viwe nanyi nyote”
(2 Wakor. 13:13)